Thursday, November 27, 2014

WATU 11 WAPOTEZA MAISHA KWENYE AJALI YA GARI LA ABIRIA BAADA YA KUGONGANA USO KWA USO NA SCANIA.


Taswira kutoka eneo la Mkanyageni baada ya ajali hiyo mbaya iliyoua watu 11.

WATU 11 wanadaiwa kufariki dunia huku wengine wakijeruhiwa katika ajali mbaya eneo la Mkanyageni mkoani Tanga baada ya gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 410 BJD kugongana na Scania namba T 605 ABJ asubuhi hii.
Katika ajali hiyo, Coaster lilikuwa likitoka mkoani Tanga kwenda Lushoto na madereva wa magari yote mawili hawajulikani walipo baada ya ajali.
Miili ya marehemu katika ajali hiyo imehifadhiwa katika Hospitali Teule ya Wilaya ya Muheza, Tanga. Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi. AMEN

No comments:

Post a Comment