Sunday, November 9, 2014

ZAO LA PAMBA LAIBUA MAKUBWA KATIKA WILAYA YA KISHAPU NI BAADA YAKUPANDISHWA BEI YA MBEGU.

Baadhi  ya madiwani wa halmashauri ya walaya  ya Kishapu  mkoani Shinyanga wakiwa kwenye kikao cha baraza la madiwani katika ukumbi wa halmashauri hiyo, ambapo suala la bei ya  mbegu za pamba zilizua mjadala mkubwa huku
wakitaka iundwe kamati ya kwenda wizara ya kilimo chakula na ushirika kufuatilia hatima ya zao hilo kutokana na bei yake kutoeleweka kila msimu na kutaka kupatiwa majibu ya kina, kwani wakulima hawana faida na kilimo hicho ikiwa ni pamoja na mbegu za pamba kupandishwa bei kutoka sh 300 hadi 500 kwa kilo moja sawa  na yanavyonunua makampuni jambo ambalo linawaumiza wakulima hali ambayo imesababisha baadhi yao kupalilia magugu ya zao hilo (maotea) shambani badala ya kuyakata.
Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Justine Sheka akizungumza kwenye kikao hicho ambapo alisema kupandishwa bei ya mbegu kunaweza kusababisha wakulima wengi kushindwa kulima zao hilo kutokana na kutoona faidia yake ,huku akiitaka serikali kulitafutiauumbuzi suala  hilo.
Kikao kinaendelea.
Wakuu wa idara mbalimbali za halmashauri hiyo wakifuatilia kwa makini michango mbalimbali iliyokuwa inatolewa na madiwani.
Baraza  linaendelea.
Maafisa tarafa wakiwa kwenye kikao cha baraza la madiwani.






No comments:

Post a Comment