Thursday, August 11, 2016

WANAFUNZI SHULE YA LITTLE TREASURES WAWATEMBELEA WAZEE,ALBINO NA WAGONJWA


Wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures iliyopo katika eneo la Bugayambele kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga wametembelea kituo cha walemavu wa ngozi (Albino) cha Buhangija katika manispaa ya Shinyanga na kuwapatia zawadi mbalimbali ikiwemo mchele,pipi,biskuti,sukari,chumvi,nguo,mafuta ya kujipaka, sabuni,miswaki na dawa ya meno ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka mitano tangu kuanzishwa kwa shule hiyo Julai mwaka 2011.

Wanafunzi hao mbali na kutembelea kituo cha Buhangija,pia wametembelea katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga na kituo cha kulelea wazee wasiojiweza cha Kolandoto katika manispaa ya Shinyanga na kuwapatia msaada kama waliotoa katika kituo cha Buhangija.

Agosti 09,2016-Wanafunzi wa shule ya Litte Treasures wakiwasili katika kituo cha walemavu wa ngozi cha Buhangija.


Shule ya Little Treasures yenye wanafunzi zaidi ya 500 imejizolea umaarufu mkubwa ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga kutokana na kuwa na mazingira rafiki ya kujifunzia kwa watoto hali inayosababisha watoto kupata elimu bora inayoendana na sayansi na teknolojia. 

Wanafunzi wakiwasili Buhangija : Shule ya Little Tresures inafundisha masomo ya Kiingereza,Kifaransa,Kiswahili na ujasiliamali ikiwemo ufugaji wa samaki,ng'ombe wa kisasa. 

Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya Little Treasures Samburu Caleb akizungumza katika Kituo cha Buhangija ambapo alisema shule hiyo imeamua kuadhimisha miaka mitano tangu kuanzishwa kwake Julai mwaka 2011 kwa kutembelea kituo hicho, kambi ya wazee Kolandoto na kutembelea wagonjwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga
Mifuko yenye vitu mbalimbali vilivyotolewa na wanafunzi wa Little Treasures

Mwalimu Caleb alivitaja vitu vilivyotolewa na wanafunzi wao katika vituo vyote vitatu kuwa ni mchele, sukari,chumvi,nguo,mafuta ya kujipaka, sabuni,miswaki na dawa ya meno vyote vikiwa na thamani ya shilingi 750,000/=

Wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures wakiwa katika kituo cha Buhangija

Watoto wenye ulemavu wa ngozi,wasiosikia na wasioona wakiwa katika kituo cha Buhangija

Wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures wakitoa burudani ya wimbo katika kituo cha walemavu wa ngozi cha Buhangija

Wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures wakiimba

Wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea kituoni

Mmoja wa walezi wa watoto kwenye kituo cha Buhangija Flora Kankutebe akiwa na watoto
Mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi,Stella Ibengwe akifurahia jambo na wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures

Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya Little Treasures Samburu Caleb akimpa mwanafunzi wake mfuko wenye sabuni,mafuta ya kujipaka,chumvi na vitu vingine vingi ili akabidhi kwa watoto wa kituo cha Buhangija 
Mlezi wa watoto katika kituo cha Buhangija akigawa pipi zilizotolewa na wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures

Mwanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures akitoa zawadi kwa mtoto mwenye albinism

Mwanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures akiendelea kugawa zawadi
Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya Little Treasures Samburu Caleb akizungumza baada ya wanafunzi wake kukabidhi zawadi zao.Kulia nimlezi wa watoto kwenye kituo hicho Flora Kankutebe 
Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya Little Treasures Samburu Caleb akiongea na watotowa kituo cha Buhangija

Magari ya wanafunzi hao 

Wanafunzi wakiwa ndani ya gari

Agosti 10,2016-Hapa ni katika kituo cha wazee wasiojiweza cha Kolandoto katika manispaa ya Shinyanga.Hawa ni baadhi ya wazee katika kituo hicho wakiwa wamekaa baada ya wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures kuwasili katika kituo hicho

Msimamizi wa kituo cha wazee cha Kolandoto Sophia Kang'ombe akiwakaribisha wanafunzi hao,ambapo alisema kituo hicho kilichoanzishwa mwaka 1917 sasa kina jumla ya wazee 14 na watoto 8

Mwenyekiti wa kituo cha Kolandoto,mzee Samora Maganga akiwa na wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures
Viongozi wa serikali ya wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures wakijitambulisha kwa wazee 

Wazee wanaoishi katika kituo cha Kolandoto
Mwalimu wa shule ya msingi Little Treasures,Alfred Mathias akizungumza kwa niaba ya uongozi wa shule hiyo
Mwalimu Alfred Mathias alisema wanafunzi wao wameamua kutoa zawadi ya chakula na mahitaji mengine muhimu baada ya kuguswa na hali ya maisha ya wazee hao kituoni
Baadhi ya vitu vilivyotolewa na watoto hao
Wazee wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea
Kaka mkuu wa shule ya msingi Little Treasures Abdillah Hamad Issa akikabidhi sabuni na dawa ya meno kwa mwenyekiti wa kituo cha wazee cha Buhangija
Zoezi la kukabidhi zawadi linaendelea
Mzee Samora Maganga akifurahia zawadi kwani ni mara ya kwanza kituo hicho kutembelewa na watoto/wanafunzi
Mwalimu Alfred Mathias akisisitiza jambo
Wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures wakiondoka katika kituo cha wazee cha Kolandoto baada ya kukabidhi zawadi ya chakula na bidhaa zingine muhimu kwa wazee hao.

No comments:

Post a Comment