Sunday, October 12, 2014

ABIRIA WAPONEA CHUPUCHUPU BAADA YA MELI YA MV VICTORIA KUNUSURIKA KUZAMA BANDARI YA KEMONDO

Meli ya Mv Victoria inayo fanya safari zake kati ya mikoa ya Mwanza na Kagera katika ziwa Victoria imenusurika kuzama karibu na bandari ya kemondo nje kidogo ya mji wa Bukoba tukio ambalo limesababisha meli hiyo kushindwa kuendelea na safari yake.
Wakiongea baada ya abiria waliokuwa  wanasafiri na meli hiyo  kutoka mjini Bukoba kwenda mwanza wamesema meli hiyo imekuwa ikipata hitilafu za mara kwa mara bila kuchukuliwa hatua na kwamba katika safari ya jana meli hiyo iliondoka mjini Bukoba saa tatu usiku lakini ilizima mara tatu ndani ya maji na hivyo ikachelewesha safari ya meli hiyo ambayo ilifika katika bandari ya Kemondo saa tisa usiku na kuleta usumbufu na wasiwasi kwa abiria waliokuwa wanasafiri na meli hiyo.
 
Kwa upande wake nahodha wa meli hiyo John Mwita amesema meli hiyo  ilipata hitilafu  kutokana na usukani kuwa mbovu  hali ambayo ilisababisha meli hiyo kuzimika mara kwa mara  na kwamba tayari kampuni ya huduma za meli imeagiza vipuri kwaajili ya matengenezo ya meli hiyo ambayo inatarajiwa kuendelea na safari baada ya matengenezo kukamilika ambapo meneja wa bandari ya Kemondo Joashi  miso  amesema meli hiyo  ilikuwa na abiria zaidi ya mia nne na hamsini na tani mia moja na hamsini za mizigo na amewataka abiria kuwa watulivu wakati taratibu za kutatua tatizo hilo zikiendelea.
 


No comments:

Post a Comment