Thursday, May 15, 2014

TUCTA YAWATAKA WALIMU KUACHA KUTUMIWA KAMA DARAJA WAKATI WA UCHAGUZI,YATOA TAHADHARI


Naibu katibu mkuu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini(TUCTA) Hezron Kaaya akizungumza akifungua semina ya elimu ya hifadhi ya jamii kwa viongozi wa vyama vya wafanyakazi mkoa wa Shinyanga katika ukumbi wa mwalimu house manispaa ya Shinyanga.
Katika hotuba yake aliwataka walimu na viongozi wa vyama vya wafanyakazi kuepuka kutumiwa kama daraja wakati wa uchaguzi na kupelekea kupatikana viongozi wasio waadilifu wala rushwa,wenye uchu wa madaraka na mafisadi hali ambayo inaweza kuipeleka nchi pabaya na kusababisha machafuko.


  

  Baadhi ya washiriki wa semina ya elimu ya hifadhi ya jamii iliyoandaliwa na mamlaka ya usimamizi wa sekta ya mifuko hiyo SSRA kutoka makao makuu jijini Dar es salaam wakisikiliza kwa makini hotuba ya mgeni rasmi.
    

 Mwezeshaji wa semina hiyo kutoka SSRA Salma Maghimbi akifafanua jinsi mamlaka hiyo inavyofanya kazi na mifuko ya hifadhi ya jamii katika kuhakikisha wanachama wake wananufaika kupitia pensheni watakazolipwa baada ya kustaafu ama kupata majanga.

  
Katibu wa chama cha walimu mkoa wa Shinyanga (CWT)Rehema Sitta akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi baada ya hotuba nzuri aliyoitoa iliyolenga zaidi kuboresha mishahara ya wafanyakazi,kurekebisha kasoro zilizopo katika malipo ya pensheni kwa wastaafu na kutoa tahadhari kwa walimu na wafanyakazi wote kuwa makini wakati wa uchaguzi wasitumiwe kupata viongozi wasio na sifa.


No comments:

Post a Comment