Sunday, October 26, 2014

YANGA KIBOKO YA STEND UNITED HIVI NDIYO ILIVYOKUWA UWANJA WA CCM KAMBARAGE SHINYANGA.

Mashabiki wa Yanga wakifurahia ushindi ni baada ya kuinyuka timu ya Stend  United goli 3-0 katika  mechi iliyopigwa   jana  uwanja  wa  CCM Kambarage mkoani  Shinyanga huku maelfu ya mashabiki wa timu hizo  wakifulika uwanjani  kushuhudia.

http://images.supersport.com/2013/5/Yanga-celebrate-300.jpg 
  Wakati timu ya Simba ikiendelea kutofanya vizuri  katika  mechi zake baada ya kulazimishwa tena sare ya bao moja kwa moja na maafande wa Prisons katika Uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, wakati mahasimu wao Yanga wakipata ushindi mnnono wa 3-0 dhidi ya Stand United mjini Shinyanga.
 
Yanga imefikisha pointi kumi baada ya kucheza michezo mitano na kuwacha mahasimu wao Simba nyuma kwa pointi tano baada ya kupata sare yake ya  tano kutokana na michezo yake mitano.
Tofauti na furaha na nderemo za Wanajangwani, Simba mambo si shwari, kwani matokeo haya mabaya sana tangu kuanzishwa kwake kwa kuambulia pointi tano kutokana na mechi tano ambayo yanaifanya timu hiyo kupoteza jumla ya pointi kumi tangu kuanza kwa msimu huu wa Vodacom Premier League.
Ilionekana kama Simba ingepata ushindi wake wa kwanza jijini Mbeya baada ya kuongoza kwa kipindi kirefu, lakini ndoto yao ilikatishwa katika dakika za majeruhi baada ya Prisons kusawazisha.
Simba ilipata bao la kuongoza kupitia kwa Mganda Emanuel Okwi kabla ya Prisons kuchomoa dakkika za majeruhi kupitia kwa Hamisi Mahingo.
 
Tofauti na matokeo ya Mbeya, Yanga imeweza kupata ushindi wake wa kwanza mnono.
Mbrazil Geilson Jaja alifungua ukurasa wa mabao katika dakika ya 13 kwa bao ambalo lilidumu hadi mwisho wa kipindi cha kwanza kisha mabao mengine mawili kufungwa  na Tegete.
 

Pichani  ni wachezaji wa Stend  United wakiwa tayari kuingia uwanjani kupambana na yanga hata hivyo waliambulia kichapo cha goli  3-0 .

No comments:

Post a Comment