Sunday, April 27, 2014

WAZAZI WATELEKEZA WATOTO KITUO MAALUMU



WAZAZI na walezi mkoani Shinyanga wameaswa kuacha tabia ya kuwatelekeza watoto wao katika kituo maalumu cha  kulea watoto  wenye ulemavu wa ngozi (Albino)wasioona na wenye ulemavu wa kusikia Buhangija manispaa ya Shinyanga,kutokana na kukua bila  kuwafahamu wazazi , wala kuelewa walizaliwa wapi nakushindwa wakati wa rikizo kwenda nyumbani.

 Akizungumza  mara baada ya kutembelea kituo hicho jana Anna Mwalongo na familia yake, kwa lengo la kutoa msaada wa chakula cha pasaka kwa watoto hao pamoja na kambi ya wazee wakoma Kilandoto,alisema inasikitisha kuona wazazi hawana uchungu na watoto wao na kukaa bila kuwakumbuka kuwajulia hali na maendeleo yao.


Anna Mwalongo ambaye pia ni muuguzi katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga ,alisema ameamua kutoa msaada wa kilo 100 za mchele,mafuta lita 20 na mbuzi wanne kwa vituo vyote viwili kwa kushirikiana na familia yake,ili kuwawezesha watoto hao  na wazee kusherehekea sikukuu ya kufufuka yesu kristo kama watu wengine badala ya kujiona kama wametengwa na jamii.

" inasikitisha mtoto kutomjua mama yake  na wala kufahamu sehemu aliyozaliwa hata wakati wa rikizo kuendelea kuishi katika eneo hili la kituoni,kutokana na  imani iliyojengeka  akirudi katika familia atauwawa, nawaomba wazazi wenzangu tuwakumbuke watoto wetu hata kuwatembelea ni faraja kubwa “mama Mwalongo.

Mlezi wa  kituo hicho Maisala Adinani alisema kuwa ,  baadhi ya wazazi na walezi wamekuwa wakishindwa kufika kuwaona watoto wao ambapo wengine tangu waletwe  imefika miaka saba hawajawahi kuwaona wazazi wao ama kuwatembelea na kuwajulia hali.

Nao baadhi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi  hamis hassan na Limi Juma waliwataka wazazi kuona umuhimu wa kurudi kuwatembelea kituoni,nasiyo kuwaacha miaka yote bila kuwakumbuka kitendo ambacho ni kuwatelekeza na kuachia jukumu hilo serikali huku wao wakisahau kabisa kama wanawatoto albino.
“Inatuuma sana inapofika muda wa kufunga shule sisi tunabaki kituoni watoto wengine wanachukuliwa na ndugu zao,hata sisi tunatamani kuwaona wazazi wetu tatizo hawajarudi tena kituoni tangu tufike ila tunamshukuru mungu kwa kuwa tunapata wageni wengi wanatutembelea na kutufariji pamoja na kutupa msaada”alisema Hassan.
Naye afisa ustawi wa jamii msaidizi wa kambi ya wazee  wakoma Kolandoto  Evodia Ndaka,alisema jamii haina budi kuiga mfano huo wa kukumbuka makundi maalumu katika jamii,kwani wanahitaji msaada zaidi kwakuwa ni wazee hawana uwezo wa kupata kipato hivyo jukumu linakuwa kwa serikali na jamii nzima.

Naibu mstahiki meya wa manispaa ya Shinyanga David Nkulila,alisema ni vema watu wakawa na upendo kwa kuwasaidia watoto na wazee pamoja na wasiojiweza,badala ya kuiachia serikali kwa kila jambo huku akipongeza hatua ya kutoa msaada wa chakula na mbuzi kutoka kwa familia ya Josephat Mwalongo na kuitaka jamii nzima kuiga mfano huo.

Zaidi ya miaka sita imepita   tangu kuanza kwa mauaji ya albino  mwaka 2007,ambapo taifa limepata doa kubwa na watu wenye ulemavu wa ngozi   takribani  72 walipoteza maisha, watu 28 walijeruhiwa  19 walifukuliwa wakiwa wamezikwa.

No comments:

Post a Comment