Sunday, May 11, 2014

MILA NA DESTURI ZILIZOPITWA NA WAKATI ZASABABISHA BAADHI YA WAFUGAJI KUHIFADHI FEDHA KWENYE MAZIZI YA NGOMBE



MILA na desturi zilizopitwa na wakati bado ni changamoto kubwa katika mkoa wa Shinyanga kutokana na baadhi ya wananchi hasa jamii ya wafugaji, kuhifadhi fedha zao kwenye mazizi ya ngombe kwa kuchimbia ardhini hali ambayo inadhorotesha uchumi wanchi kukua na kuendelea kuwa masikini.


Hayo yalielezwa  hivi karibuni na meneja wa benki ya CRDB tawi la Shinyanga Said Pamui wakati akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wadau wa habari  kwenye hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa hotel ya Diamond Fields mjini Shinyanga.

Meneja Pamui ambaye alikuwa mgeni rasmi , aliwataka waandishi kuendelea kuandika habari za kuelimisha jamii ili ijenge utamaduni  wa kutunza fedha zao kwenye taasisi za fedha, badala  ya kuweka ndani au kwenye mazizi ya ngombe huku akibainisha kuwa njia hizo siyo salama pia zinadidimiza uchumi wa nchi kutokana na fedha kutozunguka.

“Andikeni kwa kufichua maovu lakini pia na mazuri yaliyopo myaripoti  jamii ijuwe,katika mikoa ya kanda ya ziwa wananchi wengi hawana mwamko wa kuhifadhi fedha zao benki ,hii changamoto nyinyi wanahabari mnapaswa kutusaidia kutoa elimu kupitia vyombo vyenu mnavyofanyia kazi “alisema Pamuye.
Katika hatua nyingine meneja huyo alichangia rimu 50 za karatasi  kwenye stationary ya klabu ya waandishi wa habari ,ambapo  aliwataka wadau wengine kuunga mkono juhudi zinazofanywa na waandishi kuutangaza mkoa huo kwa kuripoti mara kwa mara matukio na shughuli nyingine za maendelo.
Naye mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (SPC) Shija Felician, aliwataka wadau kuendelea kutoa ushirikiano kwa vyombo vya habari wakati wa kufuatilia matukio huku hakusita kuzinyoshea kidole baadhi ya halmashauri, ambazo bado zina urasmu wa kutoa habari jambo ambalo linaminya uhuru wa kupata habari.

Alisema  bado vitendo vya kuminya uhuru wa wanahabari vinaendelea kutokea sehemu mbalimbali hapa nchini ,ikiwa ni pamoja na kunyanyaswa kwa kupigwa ,kuharibiwa vifaa vya kazi na ushirikiano mdogo kwa baadhi ya viongozi hasa wa serikali na kuwataka wandishi kutokata taama bali waongeze bidii.

Kwa upande wake mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai mkoa wa Shinyanga(RCO) Husein Kashindye ,alisema sekta ya habari ni muhimu kwa kuwa wanafikisha ujumbe sehemu kubwa kwa wakati mmoja,ambapo nguvu hiyo ikitumika kuelimisha jamiii kuachana na imani potofu za kuwa vikonge kwani nao wanahaki ya kuishi.

No comments:

Post a Comment