Sunday, May 11, 2014

ZABUNI ZA MFUKONI ZINAWATESA WANANCHI MIRADI YA MAMILION YA FEDHA YAJENGWA CHINI YA KIWANGO



UTOAJI wa zabuni kwa njia za kinyemela umesababisha baadhi ya miradi ya umwagiliaji kushindwa kutekelezeka  huku serikali ipoteza mamilion ya fedha kugharamia  miradi hiyo,  na kuwaacha wananchi wakiwa hawana matumaini ya kumalizika kero  hiyo  ili waweze kuendesha shughuli za kilimo .

Kauli hiyo ilitolewa  Naibu waziri wa kilimo chakula na ushirika Godfrey Zambi mara baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa bwawa ,katika kijiji cha Ishololo halmashauri ya Shinyanga na kukelwa na shughuli iliyofanywa na kampuni ya Syscon Builders JV Marcotech Co Ltd ya jijini Dar es salaam .

Kampuni hiyo iliingia mkataba Februari 15 ,2013 kwa jumla ya sh 940.3 milion  na wizara hiyo baada ya kushinda zabuni ,ambapo kwa sasa mradi huo umesimama kutokana na uwezo mdogo wa kifedha vifaa na kwamba ulitakiwa kukamilika 15 Dec 2013 huku vifaa vyote vya kazi vikiwa vimeharibika na kuachwa eneo la mradi.

Akiwa eneo la mradi huo Naibu waziri Zambi alisema serikali ilidhamilia kuanzisha mradi lakini mkandarasi amekuwa tatizo na hiyo inatokana na kupewa zabuni kinyemela kwani hana sifa ya kufanya kazi hiyo zaidi ya kupoteza fedha za wananchi na kuahidi kufuatilia suala hilo ili wananchi wapate bwawa.
“Nakiri wazi wizara yangu ndiyo ilifunga mkataba huu na hapa siwafichi suala hili nitalifuatilia mpaka hatua ya mwisho haiwezekani fedha za wananchi zichezewe chezewe tu,mradi umenisikitisha sana kazi iliyofanyika ni ya hovyo na tayari milon 200 zimeshatumika ,nitakaa na wataalamu wa wizara tuone cha kufanya”alisema Zambi.

Injinia wa skimu ya umwagiliaji  wa halmashauri hiyo Godfrey  Mbwambo alisema  kuwa mradi huo  ulilenga kuwanufaisha  wakulima  na wafugaji  kutoka vijiji viwili vya Ishololo na Tindeng’hulu, ambao ungeweza kunufaisha  wakulima  zaidi ya 1500 na kiasi cha hekta  zipatazo 500 kwa kumwagiliwa  maji  kutoka katika bwawa hilo.

“Mradi huu unafadhiliwa  na mradi wa uwekezaji katika sekta  ya kilimo wilaya (DASIP) ambayo ilichangia kiasi cha  zaidi ya shilingi millioni  740 na mfuko wa umwagiliaji (DIDF) kwenye mradi huo umechangia  shi  millioni 200 na kufanya jumla ya gharama  ya mradi  ya shilingi millioni 940.3”alisema  Mbwambo.

Naye  mbunge viti maalum Azzah  Hilali alisema wao halmashauri na kata hawana maelezo ya mradi huo kwa kuwa uko chini ya wizara na kumtaka mhandisi umwagiliaji kanda ya ziwa Ebenezer Kombe kutoa maelezo ya kina, kwani ndiyo wasimamizi pamoja na wizara  huku akiweka wazi kuwa wakulima  wamekuwa wakilalamika kushindwa kutekelezeka kwa wakati na kukwamisha shughuli za kilimo.
Mhandisi wa umwagiliaji ofisi ya kanda ya ziwa Ebenezer Kombe alikiri wazi kuwa utekelezaji wake hauridhishi  na kuahidi kuendelea kusimamia ili kuweza kuwasaidia wananchi kupata huduma ya bwawa na kuendesha shughuli za kilimo cha umwagiliaji.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri  hiyo Mohamed Kiyungi alimuomba Naibu waziri kiasi cha sh  200 milion  zilizotoka DIDF  na kuhamishiwa akaunti ya mradi wa DASIP Mwanza , zirudishwe kwenye akaunti ya halmashauri ili ziweze kuendeleza shughuli za miradi ya umwagiliaji.

Diwani wa kata ya Usule eneo ulipo mradi huo Amina Bundala alisema kazi hiyo ilitakiwa  ifanyike ndani ya siku 240 sawa na miezi  nane ,licha ya kuongezewa muda lakini imeshindikana na kufanya wao waonekane waongo  kutokana na majibu kwa wananchi na kupelekea mifugo  kunywa matope badala ya maji na mashamba ya   wakulima kuvurugwa  mashamba yao.

Mradi huu uliibuliwa na wananchi wenyewe katika bajeti ya kijiji  ya mwaka 2011/12  kwa kutaka bwawa kwaajili ya kilimo cha umwagiliaji  kwa zao la mpunga  ikiwa walikuwa wakikosa maji ya kutosha kwa kuliendeleza zao hilo  na kupata mavuno ya kutosha huku halmashauri ikipata pato la ndani  zaidi kupitia  ushuru za zao la mpunga.

No comments:

Post a Comment