Wednesday, July 23, 2014

HALI INATISHA KITUO CHA AFYA KAMBARAGE WAGONJWA WALALA MZUNGU WA NNE

Wakinamama wajawazito na waliojifungua wakiwa katika wodi moja kwenye kituo cha afya cha Kambarage manispaa ya Shinyanga kutokana na upungufu wa wodi,hali ambayo inaweza kuhatarisha afya zao kwa kuambukizana magonjwa. Daktari anayesimamia kituo hicho Costantine Hubby alisema
hali hiyo  imesababisha wanaweke wajawazito na waliojifungua kulala wawili wawili kitanda kimoja na wengine kulazimika kuweka magodoro sakafuni huku akitaja changamoto nyingine ni kituo kukosa chumba cha upasuaji wa dharura kwa wajawazito wenye uchungu  pingamizi pamoja na kutokuwa na gari la wagonjwa hivyo kusababisha usumbufu mkubwa mgonjwa akiwa amezidiwa hasa wakati wa msimu wa masika mvua zinaponyesha na kuwa katika hatari  iwapo atachelewa kufikishwa kwenye huduma.

Vitanda vya wagonjwa vikiwa vimefungwa kwenye mabox kutokana na kukosekana sehemu pa kuviweka kutokana na ufinyu wa wodi pamoja na upungufu.
Jengo la zahanati kijiji cha Chibe manispaa ya Shinyanga ambalo halifanyi kazi kutokana  na kukosa choo na kusababisha wanananchi wake kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya matibabu kituo cha afya cha Kambarage ambacho kinamsongamano mkubwa wa wagonjwa.
Wagonjwa wakiwa wodini
Dkt.Hubby anayesimamia kituo cha afya cha Kambarage akimueleza hali halisi ya msongamano katika kituo hicho ,katibu mkuu wa UWT Taifa Amina Makilagi hivi karibuni alipotembelea kituo hicho.


           Wagonjwa wakiwa wodini




No comments:

Post a Comment