Thursday, July 10, 2014

MIMBA ZA UTOTONI NI HATARI HIZI NDIZO ATHARI ZAKE KWA TAIFA.

Mimba za utotoni ni chanzo kikubwa cha kuongezeka kwa vifo vya watoto wachanga  kanda ya ziwa na Magharibi inayohusisha mikoa ya  Shinyanga,Mwanza,Kigoma,Tabora ,Kagera ,Simiyu,Geita na Mara taarifa ambayo ilitolewa na mtaalamu wa uzazi wa mpango kutoka mkoa wa Shinyanga Anna Mwalongo.
Alisema watoto wanaozaliwa na watoto wenzao wanakufa mapema kutokana na uangalizi kutokuwa mzuri ukilinganisha na mtoto aliyezaliwa na mama aliyefikisha umri unaotakiwa kuanzia miaka 20.
Waandishi wa habari wakiandika mpango kazi wa kufuatilia tatizo la mwitikio mdogo wa wanawake kutumia uzazi wa mpango kwa mkoa wa Shinyanga, ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo ya uzazi wa mpango kanda ya ziwa na Magharibi ambayo yamefanyika mkoani Shinyanga.
Waandishi wa habari wakiendelea na mafunzo ya uzazi wa mpango yaliyoanza juzi mjini Shinyanga ambayo yamemalizika leo.
Mratibu wa afya ya  uzazi wa mpango kanda ya ziwa Terezia Shile akifunga mafunzo ya uzazi wa mpango yaliyowakutanisha baadhi ya waandishi wa habari kutoka mikoa ya kanda ya ziwa na Magharibi,ambapo aliwataka kutumia elimu waliyoipata kwenda kuihamasisha jamii umuhimu wa kutumia njia hizo hatua itakayosaidia kupunguza idadi ya vifo vya wakinamama na watoto chini ya miaka mitano.
Waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini maelezo aliyokuwa akitoa mratibu wa uzazi wa mpango kanda ya ziwa.

Uwasilishaji wa kazi za vikundi ambazo zililenga kuainisha mtazamo potofu uliopo kwenye jamii juu ya matumizi ya uzazi wa mpango.
Waandishi wa habari kutoka mkoa wa Geita na Kigoma
Mjumbe kutoka mkoa wa Tabora akiwasilisha masuala mbalimbali waliyoyabaini juu ya uvumi na imani potofu kutumia uzazi wa mpango.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya uzazi wa mpango wakiwa katika ukumbi wa Empire Hotel mjini Shinyanga.

Waandishi wa habari kutoka mkoa wa Tabora wakiwa katika majadiliano ya namna ya kuondoa changamoto zilizopo ambazozinasababisha wanawake kushindwa kutumia uzazi wa mpango.









No comments:

Post a Comment