Monday, July 28, 2014

WANAFUNZI WANAOVAA SURUALI MLEGEZO NA VIMINI WAMKERA ASKOFU ATOA ONYO KALI

Askofu  Emanual  Makala wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania KKKT Dayosisi ya kusini mashariki ya ziwa victoria akiweka jiwe la msingi katika jengo la bweni la wavuana shule ya sekondari Mwadui wilaya ya Kishapu mkoa wa Shinyanga.           Akiwa shuleni hapo askofu Makala alisisitiza suala la maadili kwa wanafunzi na kutoa wito kwa wazazi na walezi kushirikiana kwa pamoja kuimarisha maadili kwa watoto huku akisisitiza kuwa hawatakuwa na huruma wala msamaha kwa mwanafunzi atakaye kiuka sheria za shule ikiwemo kuvaa sketi fupi,suruali mlegezo na kukutwa na simu.

 Askofu makala alisema wakishirikana ipasavyo , pamoja na kufuatilia taarifa za watoto wao shuleni itasaidia kwa kiwango kikubwa kuongeza taaluma ya wanafunzi na kupata ufaulu mzuri sanjari na kuzalisha taifa la wataalamu na viongozi wenye maadili.



Askofu Makala pia  alifungua na kuweka jiwe la msingi katika bweni Jipya la wavulana  ambalo limegharimu Sh 39 milioni zikiwa ni fedha kutoka kwa wadau wa maendeleo,wadhamini,wanafunzi pamoja na washirika wa kanisa hilo huku idadi ya wanafunzi ikiwani ni 282 kati yao wasichana ni 148 na 134 wavulana.

Askofu Emmanuel Makala akiwa katika jengo la bweni la wavulana mara baada ya kuweka jiwe la msingi pembeni yake ni mchungaji Yohana Nzelu ambaye pia ni mkuu wa shule ya sekondari Mwadui.

Ufunguzi umekamilika
Mchungaji Yohana Nzelu na viongozi wengine wakielekea eneo lilipojengwa bweni la wavulana.

Hata hivyo uongozi  wa shule ya sekondari Mwadui iliyopo ndani ya Mgodi wa madini ya Almasi( Wiliamson Diamond) wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga,umetoa onyo kali kwa baadhi ya wanafunzi wasiozingatia maadili kwa kuvaa suruali mlegezo,sketi fupi,kuwa na simu pamoja na kutumia vipodozi.

Onyo hilo lilitolewa na mkuu wa shule hiyo Mchungaji Yohana Nzelu kwenye kikao cha bodi ya shule na wazazi ,ambapo alisema hawatakuwa na msamaha kwa mwanafunzi atakaye kwenda kinyume na sheria,kanuni na taratibu walizoweka katika kuhakikisha nidhamu inakuwepo.

Shule hiyo ambayo inamilikiwa na kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Mjini Shinyanga,mbali na kuangalia maadili kwa wanafunzi pia aliwataka wazazi na walezi kuhakikisha wanafuatilia maendeleo ya watoto wao ili kuona kama wanapiga hatua.

‘’katika matokea ya kidato cha nne mwaka 2012 wanafunzi waliofanya mtihani walikuwa 61 waliopata daraja la kwanza mpaka la  tatu ni wawili mmoja alienda kidato cha tano,mwaka 2013 kiwango kilipanda walifaulu 33 kati ya 76waliofanya mtihani,waliofaulu kwenda   kidato cha tano ni 24  tukisimamia maadili ufaulu utaongezeka zaidi”alisema.



No comments:

Post a Comment