Sunday, July 27, 2014

ONA MSIMAMO WA WANANCHI ULIVYOWAPASUA KICHWA VIONGOZI KUPATA SURUHISHO LA TATIZO.

Wanachi wa kikinga maji kwenye bomba la kupampu kwa mkono ,wakati wananchi wa kijiji cha Bulekela kata ya Masanga wilaya ya Kishapu mkoa wa Shinyanga  wao wanakataa kupelekewa mradi wa maji wa aina hiyo wakiona ni kero kwao na kutaka kuwekewa mabomba ya maji hadi kwenye nyumba zao.












































HABARI KAMILI.
WANANCHI wa kijiji cha Bulekela kata ya Masanga  wilayani  Kishapu mkoa wa  Shinyanga   wameukataa mradi wa maji ambao umetengewa kiasi cha sh 28.5milion ,kutokana na kutoshirikishwa na wataalamu wakati wakifanya utafiti ,huku wao  wakitaka mabomba ya maji yasambazwe karibu na nyumba zao na siyo kuchimbiwa  visima virefu au vifupi vya kupampu kwa  mkono.

Wakati wananchi hao wakiukataa mradi huo licha ya kushauriwa na viongozi wakubwa ngazi ya mkoa na wilaya pasipo kuangalia vijiji vingine wananchi wanakabiliwa na kero kubwa ya maji,  na kumtaka mkurugenzi wa halmahauri hiyo Jane Mtagurwa kuuhamisha  mradi huo upelekwe sehemu nyingine kwani wao wameonyesha kutouhitaji .

Akizungumza  kwenye kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri hiyo diwani wa kata ya Masanga mradi ulipo Shiboka  Pombe ,alitoa kilio  chake na kusikitishwa na kitendo cha wananchi kuukataa mradi huo wakati walishirikishwa hatua zote ikiwa ni pamoja na wataalamu kutoa ushauri kuwa kuweka mabomba haitawezekana kutokana na utopatikana maji na kushauri kuwachimbia visima viwili maeneo waliyopima na kuona yanafaa.

“ Zilitengwa jumla ya sh 28.5 milion  kwaajili ya kuchimba  visima virefu lakini maji yalipokosekana kwa mujibu wa wataalamu  wetu akiwemo  mhandisi wa maji Lucas Saidi,  waliamua  viwekwe  visima vifupi  viwili kwa fedha hizo katika kijiji hicho kimoja  ambavyo vitatumia  pampu ya mikono”alisema Diwani Pombe.

Akichangia hoja hiyo  diwani wa  kata ya  Mwamashele Julius Kwihuja  alisema   maazimio yalikuwa  mradi huo uhamishwe  kwani maeneo mengi wananchi wanateseka kwa kukosa huduma ya maji ,halafu  wao  wamepata kiburi  kwanini wabembelezwe  ni vema ukahamishwa kwani tayari suala hilo limeshafikishwa kwenye  kamati ya maji na kuzungumzwa kuwa mradi huo uhamishwe kutokana na kujivunia kuwa karibu na mto.

Hata hivyo mwenyekiti wa  halmashauri hiyo  Justine Sheka alisema kuwa utafiti uliopatikana hapo kuwa eneo hilo  maji ni kidogo ila eneo walilochimba kisima maji yapo kwa wingi  ila wao bado hawataki  hata mradi ukihamishwa tayari kunahasara  manunuzi ya pambu ni shilingi million saba,gharama ya uchimbaji shilingi million 20 tayari zimekwisha tumika.

Pia mhandis wa maji Saidi  awali alidai kuwa  walipopima eneo hilo  walibaini  maji ni kidogo kwa kutotosheleza mtandao wa maji ya pomba kwa kitaalamu   hivyo wakashauri kuwa kuwekwe visima vifupi vya pambu ya mikono lakini wananchi walipoelezwa walikataa na kutaka mabomba yatakayo sambaaa mpaka majumbani mwao.

Naye mkurugenzi wa halmashauri hiyo  Jane Mtagurwa alisema kuwa  malalamiko yaliyopo dhidi ya wananchi kuwa wakati wataalamu wanapima hawakushirikishwa ,hivyo mpango wa upimaji uanze upya  kwa kuwashirikisha ikiwa utaratibu wa kusambaza mabomba  ufanyike,wanachokataa kingine ni ile shida ya kupampu kwa mkono.

“Kuhamisha mradi huo utaleta tena gharama kubwa  hakuna fedha  kinachotakiwa  ni kuondoa  mgogoro uliopo,mpango wa upimaji uanze upya  kwa kuwashirikisha  wananchi na usambazaji wa  maji kwenye mambo ufanyike shida yao hawataki visima hivyo ambavyo vya kupampu kwa mkono ndicho kilichobainika kwenye kijiji hicho”alisema mkurugenzi  Mtagurwa.

 Na Stella Ibengwe.

No comments:

Post a Comment