Saturday, August 2, 2014

CHANZO CHA MADIWANI WAWILI WA CHADEMA KUHAMIA CCM KISHA KURURUDI CHADEMA, ILIKUWA HIVI SOMA STORI KAMILI

Ikiwa ni miezi mitano tu tangu wavuwe magwanda ya CHADEMA mbele ya Nape Nauye wa CCM  huku maelfu ya wananchi wakishuhudia,ndivyo ilivyotokea tena Julai 30 mwaka huu madiwani hao wamevua pia nguo za CCM na kurudia Magwanda.

Katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi Nape akiwatambulisha  madiwani hao mara baada ya kutangaza kutoka CHADEMA na kujiunga CCM  wakiwa jukwaani katika viwanja vya mahakama nguzonane ilikuwa ni february 25 mwaka huu siku waliyojiuzuru na kuhamia CCM baada ya siku tatu.
Hii ndiyo habari kamili.


MADIWANI wawili wa chama cha Demokrasi na maendeleo (CHADEMA)waliojiuzuru nyadhifa zao mapema mwaka huu kisha kujiunga na CCM, hatimaye wamerudi tena Chadema huku wakitoboa siri iliyofanya waondoke kuwa waliahidiwa watapelekwa chama kipya cha Alliance for Change and Transparency (ACT- Tanzani na kudai kuwa mpango huo ulihusisha vigogo wengine wa chama hicho.



Wakizungumza jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya mahakama ya mwanzo manispaa ya Shinyanga ulioandaliwa na CHADEMA,madiwani hao waliojiuzuru Sebastian Peter kata ya Ngokolo na Zacharia Mfuko  kata ya Masekelo walisema wao walikuwa ni watu wa kwanza kuondoka lakini mikakati hiyo waliipanga na viongozi wengine kubwa ndani ya chama ili wakajiunge na chama kipya cha ACT waweze kukijenga.



Sebastian alisema baada kuondoka walijua wataingia moja kwa moja ACT lakini hali ilikuwa tofauti kutokana na kutakiwa kujiunga kwanza CCM ndipo wapate nafasi ya kwenda huko,jambo ambalo waligundua kuwa wamechezewa kamali kisha kuamuwa kurudi  kuwaomba msamaha wanachama na wananchi ili wawapoke kwani walichobaini ni michezo ya kisiasa ya kutaka kuharibiana.



“Ninashangaa sana kuona hapa viongozi wengine wanatuponda wakati wote tulikuwa kwenye mkakati huo wa kuondoka Chadema kwenda ACT, sisi tulitangulia kwenda kuangalia mazingira kama ni mazuri ili na wao wafuate lakini tulichokikuta huko mmbo siyo mazuri ninawasihi achaneni na mpango huo huko hapafai bora Chadema na ndiyo maana tumerudi”alisma Peter.



Hata  hivyo mara baada ya kufika eneo la mkutano madiwani hao waliojiuzuru  waliamsha hasira kwa wananchi na wanachama ambao waitaka waondoke eneo hilo kwa kuwa ni wasaliti wakubwa wa Chadem, hivyo hawahitaji kuwaona,ndipo mbunge wa chama hicho jimbo la Maswa mashariki Sylivester Kasulumbayi ilimlazimu kuingilia kati kuwatuliza kisha mkutano kuendelea.



Madiwani hao walifika kwenye mkutano huo wakiwa wamebebwa kwenye piki piki huku wamevaa sare za CCM baada ya wanachi kushusha hasira waliwapa fursa ya kujieleza kila mmoja,kisha waliondolewa kwa gari kabla mkutano haujaisha kwa ajili ya usalama wao ili kuepusha vurugu kutokea.



Naye Zacharia Mfuko mmoja wa waliojiuzuru alilihusisha tukio la kuondoka kwake kuwa zilitumika nguvu za giza kuwachanganya akili na kuamuwa kuondoka Chadema ,kwani mpaka sasa anajutia hatua aliyoichukuwa ya kwenda CCM na kuwaomba wanachama wampokee kwa kuwa bado ana mambo mengi ya kueleza mchakato ulivyokuwa ukifanyika wa kukibomoa chama hicho.



Alisema kuna baadhi ya viongozi wa CCM wakubwa walihusika katika kuwarubuni ili wahamie huko na baada ya kufanikiwa kuwapata waliwachukuwa wakawapeleka jijini Dar es salaam ambako walikutana na viongozi wengine kisha kurudishwa Dodoma na kuendelea na mikakati ya kupata wanachama wengi zaidi watakaokwenda kuijenga  ACT.


Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Maswa mashariki Sylvester Kasulumbayi aliwataka wananchama wa Chadema kuwapokea huku akisema walirubuniwa na kwamba hatua hiyo itawawezesha kufahamu zaidi mambo yaiyokuwa yamejificha ili waweze kuyafanyia kazi ili kukijenga chama na kuwa imara zaidi badala ya kuwa na mpasuko.

“Ndugu zangu mhalifu akikamatwa huwa hawamuuwi unamuacha ili akupe taarifa zaidi za wahalifu wengine kwa hiyo na mimi ninawaomba sana  wanachadema wenzangu  tuwapokee walifanya hivyo kimakosa,tusiwe na hasira  ili tuweze kufahamu mambo mengi zaidi yaliyokuwa yamejificha”alisema Kasulumbayi.


Madiwani  hao walitangaza  rasmi kujiuzuru nyasifa zao mwezi februari mwaka huu  kutokana na madai ya uongozi ngazi ya taifa  kuendelea kusikiliza majungu,kudhalilisha baadhi ya viongozi  pamoja na  kuwaita  wahaini na wasaliti ndani ya chama na baadaye walijiunga na CCM.
                           
Na Stella blog.


No comments:

Post a Comment