Saturday, August 2, 2014

HII NI HATARI,UHALIFU WA AINA YAKE WAIBUKA NCHINI WAUAJI WAKUKODI

Mitandao ya kihalifu inazidi kujiimarisha nchini na sasa kumeibuka makundi ya wauaji wa kukodi katika mikoa ya kaskazini mwa nchi pamoja na Kanda ya Ziwa.

Mbali na mauaji ya albino na vikongwe ambayo yalipata kutikisa katika maeneo kadhaa ya nchi, wauaji wa kukodi wanatumika kutekeleza uhalifu huo kwa lengo la kulipiza kisasi, uporaji wa fedha, kujitanua kibiashara au kudhulumu mali na fedha.

Uchunguzi wa muda mrefu uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa silaha nyingi zinazotumika katika mauaji ya kukodi yanayofanyika mikoa ya Kanda ya Kaskazini, hununuliwa ama kukodishwa kutoka Namanga upande wa Kenya.

Wauzaji wa silaha hizo ni ama raia wa Kenya wenye asili ya Kisomali ama wahamiaji haramu wenye asili ya Kisomali wanaoingia nchini, wakitokea Somalia kupitia Kenya.

Uchunguzi umebaini kuwa bunduki aina ya Submachine Gun (SMG) huuzwa kati ya Sh3 milioni hadi Sh5 milioni na bastola zikiuzwa kati ya Sh500,000 na Sh1.2 milioni.

Pamoja na kutoka nje ya nchi, wauaji wengine wa kukodi hupatikana nchini kulingana na aina ya mtu wa kuuawa, mazingira na ugumu wa kazi.

Kwa Tanzania, mikoa inayoongoza kwa kuwa na wauaji wa kukodi ni Arusha na Manyara na Mkoa wa Kilimanjaro umekuwa ukiguswa kuwa jirani na mikoa hiyo.

Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina, mtoa taarifa wetu alisema alisema: “Hata sasa ukihitaji vijana wa kazi nitakuunganisha. Jambo muhimu hakikisha huwarushi (unawapa fedha zao), ukiwarusha lazima na wewe watakuua.”

“Yupo rafiki yangu anayewafahamu vyema kwa sababu amewahi kuwaunganisha na waliokuwa wakihitaji huduma yao,” alisema mtoa habari huyo.

Malipo ya kuua

“Malipo kwa kazi hii yanaanzia kati ya Sh1 milioni na Sh5 milioni kutegemea na uzito wa kazi husika,” alisema mtoa taarifa wetu anayeishi Arusha na akithibitisha kwamba anafahamiana na madalali wa wauaji hao.

Alisema mara nyingi wauaji hao hawataki kukutana na wateja moja kwa moja ili kuepuka kutambulika, badala yake hukutana au kuwasiliana na mtu wa kati (wakala) ambaye pia hupokea malipo na kuwakabidhi
VIA:  Mwananchi.

No comments:

Post a Comment