Friday, February 7, 2014

MWALIMU AJINYONGA KWA KAMBA YA KATANI CHOONI,KISA MSONGO WA MAWAZO

MSONGO wa mawazo umesababisha mwalimu wa shule ya msingi  Mwang’osha iliyopo kata ya nyamalongo wilaya ya shinyang mkoani hapa  Christipian Mafuru (24),kufariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia kamba ya katani katika choo cha nyumbani kwake.
Akizungumzia tukio hilo  mwalimu mkuu wa shule hiyo Frida Maleko alisema mwili wa mwalimu huyo ulikutwa  juzi majira ya saa tisa na nusu alasiri akiwa amejinyonga baada ya kukaa muda mrefu bila kumuona shuleni.
 Mwalimu mkuu alisema baada ya kukaa muda bila kumuona ndipo  alichukua jukumu la kumpigia simu ambayo iliita bila ya kupokelewa  na kuamua kuondoka na walimu wenzake kwenda nyumbani kwake  ambapo walikuta  mlango umefungwa.
Kufuatia hali hiyo  iliwatia mashaka na kuamuwa  kuvunja dirisha la nyumba hiyo ambapo hawakukuta  mtu  ujumbe wa maneno ulioandikwa kwenye  Barua na kuwekwa mezani uliokuwa umeandikwa na marehemu.
Ujumbe huo ulikuwa ukisomeka  kuwa ‘’Msongo wa mawazo umenilazimu nifanye hivi, poleni sana walimu wenzangu,samahani wazazi wangu,kwa heri mwanagu Ray” hali ambayo iliwatia hofu kubwa.
Mwalimu mkuu alisema Marehemu aliajiriwa mwaka jana  kwenye shule hiyo  na alikuwa mchapakazi  aliomba zamu zote za walimu azifanye yeye ili apate uzoefu wa kazi, lakini walishituka baada  ya kutomuona muda mrefu shuleni .
“Tulipomkosa  nyumbani kwake na kuona ujumbe ambao ulitutisha  tulishauriana  na walimu wenzangu tukaona ni vema tumtafute hivyo kuchukua jukumu la kuanza kumtafuta na ndipo tuliukuta mwili wake ndani ya choo kajinyonga na ikabidi kutoa taarifa  polisi”alisema Mwalimu Maleko.
kamanda wa jeshi la polisi mkoani shinyanga kamishina mwandamizi wa jeshi la polisi (SACP) Evarist Mangala, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akisema chanzo cha  kifo hicho ni msongo wa mawazo wa mwalimu huyo kutokana na barua aliyoandika yeye mwenyewe kwa mkono wake na kutia saini .
Katika tukio hilo  hakuna mtu aliyeshikiliwa na jeshi la polisi kuhusiana na  kifo hicho,ambapo mwili wa marehemu  umeagwa jana shuleni hapo na kusafirishwa   kwenda nyumbani kwao wilayani sengerema mkoani mwanza  kwa mazishi.

No comments:

Post a Comment