Saturday, June 21, 2014

WALINZI WA MGODI WA MWADUI WAUA KISHA KUTELEKEZA SILAHA NA KUKIMBIA,HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA JIONEE PICHA HALISI



MKAZI mmoja wa kijiji cha Masuguru kata ya Mwaduiluhumbo wilaya ya Kishapu aliyefahamika kwa jina la Juma Masalu (25) , ameuawa kwa kupigwa risasi  baada ya kuvamia ndani ya mgodi wa madini ya Almasi, unaomilikiwa na kampuni Wiliamson Diamond akiwa na wenzake 20 kwa lengo la kuiba mchanga unaosadikiwa kuwa na madini.


Tukio hilo lilitokea Juni 13 mwaka huu majira ya saa 5:00 usiku kufuatia kundi hilo kuvamia mgodi wakiwa na silaha za jadi mishale,mikumi,makombeo ya kurusha,ndipo walinzi wa kampuni ya Zenith wanaolinda mgodi huo walijihami kwa kupiga risasi za moto na kusababisha mauaji hayo na mmoja kujeruhiwa mguuni huku wengine wakikimbia.

Matukio ya uvamizi kama huo yanayofanywa na vijana wanaojiita wabeshi yamekuwa yakitokea mara kwa mara ,ambapo mwaka jana kundi la watu zaidi ya 100 walivamia mgodi huo wakiwa na silaha za jadi wakitaka kuchukua mchanga wa almasi na kusababisha wawili kujeruhiwa na kupata ulemavu wa maisha baada ya kukatwa miguu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na kaimu kamanda wa jeshi la polisi mkoani shinyanga , Kihenya Kihenya alisema walinzi walianza kupambana nao kwa kuwa rushia risasi, huku wavamizi hao wakirusha  silaha za jadi walizoingia nazo na baadaya kuzidiwa nguvu  walikimbia na mwenzao kupoteza maisha papo hapo aiyepigwa risasi sehemu za siri.

Kaimu kamanda alimtaja aliyejeruhiwa kwa risasi kuwa ni Emmanuel Charles (23) mkazi wa kata ya  majimaji mji wa maganzo,ambaye alipigwa risasi mguu wa kushoto kisha kukamatwa  na kupelekwa katika zahanati ya Mgodi huo kwa kupatiwa matibabu huku akishikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano zaidi.

Kufuatia tukio hilo la mauaji kutokea walinzi wawili wa kampuni ya Zenith ambo majina yao hayafahamika, waliokuwa wakipambana na wavamizi hao wanaofahamika kwa  jina la Wabeshi walikimbia kusiko julikana  wakihofia kukamatwa na kuzitelekeza  bunduki zao.

Jeshi la polisi mkoani humo linawatafuta wavamizi wengine kumi na nane waliokimbia mara baada ya kuzidiwa  kwa mashambulizi ya silaha za moto iliwaweze kutiwa nguvuni na kufikishwa katika vyombo vya sheria na kuwataka vijana kutafuta shughuli zingine na siyo kuvamia mgodi kutafuta madini.

Matukio ya uvamizi kama huo yanayofanywa na vijana wanaojiita wabeshi yamekuwa yakitokea mara kwa mara ,ambapo mwaka jana kundi la watu zaidi ya 100 walivamia mgodi huo wakiwa na silaha za jadi wakitaka kuchukua mchanga wa almasi na kusababisha wawili kujeruhiwa kwa risasi  na kupata ulemavu wa maisha.

No comments:

Post a Comment