Saturday, July 5, 2014

BIASHARA YA MAGENDO YA NGOZI KUDHIBITIWA NI BAADA YA SERIKALI KUANZISHA MFUMO WA UFUATIIAJI.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Mwanvua Jilumbi akifungua warsha ya wadau wa ngozi Mkoani Simiyu, iliyokuwa na lengo la kujadili mfumo mpya wa kukusanya ushuru unatokana na zao la ngozi.   akifungua warsha hiyo katibu tawala huyo alieleza kuwa mkoa wa simiyu kwa mwaka 2013/14 hakuna hata senti moja ilikusanywa kutokana na ushuru wa ngozi, licha ya mkoa huo kuwa na idadi kubwa ya mifugo kama ngo'mbe, mbuzi, pamoja na kondoo.   alisema kuwa idadi kubwa ya wafugaji wamekuwa hawatozwi ushuru pindi wanapoleta ngozi zao kuwauzia wafanyabishara wanaosafirisha zao hilo nje ya nchi. sambammba na hayo Jilumbi alieleza kuwa Mkoa wa Simiyu una idadi ya ng'ombe wapatoa Milioni 1.5 idadi aliyosema kuwa inalingana na watu walioko mkoani hapa.

alisema kuwepo kwa magendo ya bishara ya zao hilo imekuwa changamoto kubwa inayosababisha serikali kukosa ushuru unaotokana na ngozi, ambapo aliwataka washiriki wa warsha hiyo kujadili kwa kina jinsi ya serikali inatakavyokusanya ushuru unaotokana na zao hilo.






Washiriki wa warsha hiyo wakimsikiliza mgeni rasmi Katibu Tawala wa Mkoa wa simiyu Mwanvua Jilumbi wakati akifungua warsha.



Picha na Simiyu news Blog

No comments:

Post a Comment