Sunday, July 20, 2014

USAFIRI WA DALADALA ZA BAISKELI KUPIGWA MARUFUKU MANISPAA YA SHINYANGA

Baadhi ya waendesha daladala za baiskeli manispaa ya Shinyanga wakiondoka eneo la mkutano .Picha kwa  hisani ya Malunde blog.  
STORY KAMILI.
KUTOKANA na kukithiri  vitendo vya ukatili  kwa watoto wadogo kubakwa kisha kutoborewa macho na baadhi ya waendesha daladala za baiskeli,baraza la madiwa la manispaa ya Shinyanga   limeazimia  kuziondoa  daladala zote za baiskeli maeneo ya mjini   ili kukabiliana tatizo hilo pamoja na ajali huku zaidi ya matukio matano ya ukatili yameshatokea.

Baraza hilo lilifikia uamuzi huo katika kikao chake kilichofanyika jana baada ya mchumi wa manispaa hiyo Christopher Nyarubamba, kutoa taarifa ya kamati ya uchumi,afya na elimu  wakishauri kuondolewa daladala hizo kata za katikati ya mji na kutakiwa kuwa   kando ya mji kwa kupatiwa  usajili  na kupewa vitambulisho  pindi yanapotokea  mtukio iwe rahisi kuwabaini.

Taarifa hiyo ya kamati  alishauri kuondoa daladala na kutaja sababu za msingi huku madiwani wakiunga mkono azimio hilo na kuwataka wananchi wa manispaa  kubadilika kama maeneo mengine  kutumia daladala za magari kama ilivyo katika maeneo mengine kwani niaibu mpaka sasa mji mzima  unatumia daladala za baskeli wakati inaitwa manispaa.

Wakichangia  hoja hiyo baadhi ya madiwani  Siri Yasin (CHADEMA) na  Shella  Mshandete  (CCM) walisema  hakuta wezekana kuwafukuza  waendesha  daladala za baiskeli bila kufahamu  mbadala wake,hivyo inatakiwa usafiri upatikane ndipo zoezi la kuwaondoa lianze ,kwani ndiyo tegemeo kubwa la usafiri waliouzoea  wananchi  hivyo kuwakatisha ghafla italeta tatizo.

“Hili jambo halipingiki ni kweli kuna kero na kunamatukio mengi ya ukatili wa watoto yametokea kwa kusababishwa na wandesha daladala,lakini mimi ninashauri tutafute kwanza mbadala kabla ya kupiga marufuku daladala hizo,manispaa ikae na wamilii wa magari kuona namna ambavyo wanaweza kutoa magari yakaanza kusafirisha watu mitaa ya mjini”alisema Shella.

Katibu tawala wa wilaya ya Shinyanga Boniface Chambi  alisema kuwa  daladala za gari zilikuwepo  na uzinduzi ulifanywa na mkuu wa mkoa Ally Rufunga , lakini cha kushangaza  watu walikuwa hawapandi hali iliyowakatisha tamaa wenye daladala hizo na kuamua kusitisha  mpaka sasa na kuendelea  kuonekana daladala za baiskeli pekee.

Awali  Naibu  mstahiki meya wa manispaa hiyo David Nkulila alisema kuwa   daladala  za baiskeli ziondolewe kama lilivyopitishwa azimio,huku akiwanyoshea kidole  baadhi ya askari wenye tabia ya kukamata magari ya abiria hovyo  wakilenga  mitazamo yao ya kimaslahi kuwa  halitavumiliwa na kuwataka kuchukuwa hatua pindi gari linapokuwa na tatizo.

No comments:

Post a Comment