Friday, August 8, 2014

SHEREHE ZA NANENANE ZA TIKISA SHINYANGA HIVI NDIVYO HALI ILIVYOKUWA

Mambo ya TBL hayo,akinamama walijitokeza kucheza taarabu uwanjani hapo katika kusherehekea sikukuu ya wakulima nane nane mkoani Shinyanga.
 
Hapa ni katika uwanja wa ccm Kambarage mjini Shinyanga ambako leo kumefanyika sherehe ya wakulima kubwa zaidi likiwa ni mashindano ya mbio za baiskeli kwa kanda ya ziwa na mashariki ambayo yamekutanisha mikoa ya Geita, Kagera, Mara, Mwanza, Tabora, Shinyanga na Simiyu chini ya udhamini wa TBL kupitia bia yake ya Safari Lager.Pichani ni wachezaji wa ngoma ya Mabhulo kutoka Ishinabulandi mkoani Shinyanga wakifanya yao uwanjani.Pamoja na ngoma za jadi pia show za kila aina zilikuwepo
Vijana waliojitokeza kuonesha uwezo wao wa kucheza wakishambulia jukwaa katika uwanja wa CCM Kambarage leo mjini Shinyanga
Mshindi wa kwanza mbio za kilomita 15o kutoka Shinyanga kwenda Isaka na kurudi Shinyanga Martha Anthony kutoka Mwanza akiingia uwanjani leo,Martha kajinyakuliash ilingi laki 7.
Vijana matata kutoka Shinyanga"Wakali Kwanza wakionesha show uwanjani leo.
Kushoto ni mshindi wa kwanza katika mbio za kilomita 220 kutoka Shinyanga kwenda Kahama na kurudi Shinyanga Goleha Ngusa kutoka kutoka Simiyu ambaye ameondoka na kitita cha shilingi milioni moja,kulia kwake ni mshindi wa pili Daudi Helemala kutoka Mwanza,ambaye ameondoka na shilingi laki 8.  
Mashindano ya mbio za baiskeli kwa kanda ya ziwa na mashariki yamefanyika  katika mkoa wa Shinyanga yamefanyika leo katika uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga yakiwa yamedhaminiwa na TBL kupitia bia yake yake ya Safari Lager huku mgeni rasmi akiwa ni kaimu katibu tawala msaidizi utawala na utumishi bwana Raymond Kiwesa kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga.

Michezo ya mbio za baiskeli iliyofanyika ni mbio za masafa marefu kwa wanaumme kilomita 220 kutoka Shinyanga kwenda Kahama na kurudi Shinyanga,mbio kwa akina mama kilomita 150 kutoka Shinyanga hadi Isaka na kurudi Shinyanga,mbio za watu wenye ulemavu kilomita 12(kuzunguka uwanja wa kambarage mara 30),mbio za akina mama wakiendesha baiskeli wakiwa wamebeba ndoo kichwani,ngoma za asili pamoja na show mbalimbali.

Akitangaza washindi katika mbio hizo za baiskeli,katibu wa chama cha baiskeli kanda ya ziwa mashariki John Elisha amesema mbio za baiskeli kwa upande wa wanaume kilomita 220 wametumia masaa 6 na dakika 6 kutoka Shinyanga kwenda Kahama na kurudi Shinyanga.

Amemtaja mshindi wa kwanza katika mbio hizo kuwa ni Goleha Ngusa kutoka kutoka Simiyu ambaye ameondoka na kitita cha shilingi milioni moja,mshindi wa pili Daudi Helemala kutoka Mwanza,ambaye ameondoka na shilingi laki 8,mshindi wa tatu Simon Mbaruku kutoka Simiyu,ambaye amjenyakulia shilindi laki 6,mshindi wa nne ni Masunga Duba kutoka Mwanza ambaye amejinyakulia laki 5 na mshindi wa tano Nchuki Samweli kutoka Shinyanga ambaye ameondoka na shilingi laki 3 huku washindi wa 6 hadi 10,laki 1 kila mmoja,washindi wa 11 hadi 20 kila mmoja shilingi elfu 50.

Kwa upande wa mbio za baiskeli kwa akinamama  kilomita 15o kutoka Shinyanga kwenda Isaka na kurudi Shinyanga mshindi wa kwanza ni  Martha Anthony kutoka Mwanza ambaye ameondoka na shilingi laki 7,mshindi wa pili Salome Donald kutoka Shinyanga,ameondoka na shilingi laki 5,wa tatu Laurencia Luzuba kutoka Mwanza aliyejinyakulia shilingi laki 3,mshindi wa nne Elizabeth Donald kutoka Shinyanga alipata laki 2 na mshindi wa 5 ni Elizabeth Clement kutoka Shinyanga ambaye ameondoka na shilingi laki 1 na nusu huku mshindi wa 6 hadi 10 kila mmoja akiondoka na shilingi laki 1 na wa 11 akiondoka na shilingi elfu 50 kama kifuta jasho chake.

Katibu huyo wa chama cha baiskeli kanda ya ziwa mashariki amemtaja mshindi wa kwanza kwa kwa upande wa mbio za akinamama wanaoendesha baiskeli wakiwa na ndoo kichwani kuzunguka uwanja wa Kambarage kuwa ni Makirikiri Joseph ambaye amejinyakulia shilingi laki moja na nusu,mshindi wa pili Christina Giti ambaye amepata shilingi laki 1,mshindi wa tatu Joyce Bundala aliyejinyakulia shilingi elfu 80,mshindi wa nne Tatu Hassan aliyepata shilingi elfu 60,wa nne Jenny Shaban aliyeondoka na shilingi elfu 50 huku mshindi wa 6 hadi 12 akiondoka na shilingi elfu 30 kama kifuta jasho chao wote kutoka Shinyanga.

Kwa upande wa mbio za baiskeli kwa watu wenye ulemavu kuzunguka uwanja wa Kambarage mara 30,mshindi wa kwanza ni Makende Derema aliyejinyakulia shilingi laki 1 na nusu,mshinidi wa pili Ngalu Ngamba aliyondoka na shilingi laki 1,mshindi wa tatu Peter Thomas aliyejinyakulia shilingi elfu 80,mshindi wa 4 Gogadi Shija aliyeondoka na shilingi elfu 60 na mshindi wa 5 Shija Nkwabi aliyeondoka na shilingi elfu 50.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi hizo kwa washindi wote mgeni rasmi kaimu katibu tawala msaidizi utawala na utumishi bwana Raymond Kiwesa kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga ameipongeza kampuni ya bia bia ya TBL kwa kuwa mstari wa mbele katika kudhamini mashindano hayo na kuwaomba waendelee kusaidia sekta ya michezo pamoja na kwamba kila mara wamekuwa wakidhamini michezo ya aina mbalimbali kama vile mpira wa miguu,pool table.

Kwa upande wake meneja mauzo na usambazaji TBL kanda ya ziwa bwana Malack Sitaki amesema miongoni mwa  malengo ya TBL kudhamini mbio hizo za baiskeli ni kuhamasisha michezo nchini,kuwa karibu na wateja wake wa bia ya Safari Lager kutoa burudani kwa wananchi ukiangalia wananchi wengi mkoani Shinyanga na kanda ya ziwa kwa ujumla wanapenda mbio za baiskeli.

Huu ni mwaka wa 16 tangu TBL kupitia bia yake ya Safari Lager na mwaka huu washiriki walikuwa wanatoka mikoa ya Geita, Kagera, Mara, Mwanza, Tabora, Shinyanga na Simiyu.
Na Malunde1 blog.
    

No comments:

Post a Comment