Monday, September 1, 2014

KADA WA CCM MBARONI KWA UBAKAJI NA UJAMBAZI

JESHI la Polisi mkoani Simiyu linamshikilia kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ramadhani Busega ambaye ni Mwenyekiti wa Kata ya Mawamanyili
, wilayani Busega kwa tuhuma za ujambazi na ubakaji.

Pia linaendelea kumsaka Mchumi wa CCM Wilaya ya Busega, Mashaka Obedi ambaye anadaiwa kukimbia baada ya kufanya uporaji wa sh milioni 20 katika nyumba ya Mwalimu Samwel Mkumbo anayeishi kitongoji cha Nassa Ginnery, Kijiji cha Mwagulanja wilayani humo.

 Baada ya kupora inadaiwa walivamia chumba cha mwalimu mwingine ambaye alikuwa amepanga kwenye nyumba hiyo na kumbaka.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Charles Mkumbo, Msoka na wenzake walidaiwa kufanya tukio hilo saa 7 usiku kuamkia Agosti 28 mwaka huu, kijijini humo na kisha kutoweka, ambako Jeshi la Polisi limewatia nguvuni 
baadhi na kuendelea kumsaka mchumi huyo wa CCM.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kwa njia ya simu, Kamanda Mkumbo, alisema ni kweli tukio hilo limetokea na watu wengine kadhaa wanashikiliwa.

Kamanda Mkumbo, aliwataja wengine wanaoshikiliwa ni Libent Rwegarulila ambaye ni Mshauri wa Mahakama ya Mwanzo ya Nyashimo wilayani Busega, Mkurugenzi wa NGO’s moja inayojishughulisha na masuala ya wazee wilayani Magu, Nkondo Kubini na Meshack Samson ambaye ni mfanyabiashara wa duka la rejareja kijijini hapo, wote wakiwa wakazi wa Nassa Ginnery.

Alisema kwamba, watuhumiwa hao walipomvamia mwalimu huyo walimpora sh milioni 20 kabla ya kuingia katika chumba cha mpangaji wake ambaye pia ni mwalimu na kumbaka kwa zamu.

Hata hivyo, alisema wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na kwamba hatosita kumfikisha mtu katika vyombo vya sheria kutokana na kosa walilofanya, hata kama wametoka katika chama tawala kwa kuwa viongozi wanatakiwa kuwa mfano na si kufanya mambo mabaya katika jamii.
Chanzo :Tanzania daima

No comments:

Post a Comment