Friday, September 5, 2014

MAGARI MATATU YAMEGONGANA USO KWA USO BUTIAMA MKOA WA MARA NA KUUA WATU ZAIDI YA 30 NA KUJERUHI 80

 Kufuatia ajali mbaya iliyohusisha magari matatu wilayani Butiama mkoani Mara idadi ya watu waliopoteza maisha ni 38 hadi sasa huku majeruhi wakiwa ni 80.

Kwa mujibu wa mkuu wa wilaya ya Butiama  Anjelina Mabula aliyezungumza na TBC muda mfupi uliopita ajali hiyo amesema ajali hiyo imehusisha basi la AM Coach lenye namba za usajili  T736 AWJ likitoka Musoma kwenda Mwanza limegongana uso kwa uso na basi T677 CYC J4 Express likitoka Mwanza kwenda Tarime na gari jingine dogo aina ya Nissan Corola P332 KKT

 likitoka eneo la Sabasaba yote yalikutana kwenye mteremko yakitokea juu kwenda Darajani katika kupishana hawakuweza kupishana yakagongana na wakati huo gari dogo likapaki pembeni nalo likagongwa kwa nyuma likasukumwa na kutumbukia mtoni.

Katika gari dogo kulikuwa na watu 8,wawili wamefariki dunia na majeruhi 36 kutoka kwenye mabasi nao wamefariki na majeruhi 80 wamekimbizwa katika hospitali ya mkoa wa Mara.

Madereva wote wamefariki dunia,na kwamba mizigo ya majeruhi iko chini ya ulinzi wa polisi

No comments:

Post a Comment