Thursday, September 4, 2014

VIONGOZI WAKATAZA DENSI YA UNENGUAJI VIUNO NA TUMBO

Viongozi wakataza unenguaji viuno

Densi ya kunengua viuno na tumbo ya 'Belly Dance nchini Misri
Bodi ya kidini ya misri, imetoa fatwa kukataza uonyeshaji wa kipindi kilichoanzishwa kwenye televesheni nchini humo kuonyesha densi ya jadi ya wanawake wa misri ya kunengua viuno
almaarufu 'belly dance'.
Ngoma hiyo inayofanana na chakacha ya waswahili imechezwa tangu zama za kale na imenakiliwa hata katika enzi za ma-pharoah katika nchi hiyo ya Misri.
Ni densi ambayo isingekosekana kwenye sherehe muhimu. Harusi au burudani nyenginezo.
Maelfu ya watalii wanaoitembelea Misri hupenda kwenda kuona inavyochezwa lakini mnamo siku za hivi karibuni wasichana kutoka sehemu nyingi duniani hasa ulaya na hata uchina wameripotiwa kwenda Misri kujifundisha jinsi ya kucheza densi hiyo.
Ni ajabu kuwa sasa imekuwa maarufu katika mataifa ya kigeni kuliko Misri kwenyewe ambako haichezwi ovyo ovyo hadharani.
Misri ni nchi ya waislamu wengi hivyo burudani zina miiko yake- densi kama hizo hazichezwi hadharani hasa kwenye mikusanyiko ya umma ya mchanganyiko wa wake kwa waume.

Hivi wale wanaozishabikia ni wachache kiasi kuwa sasa kuna hofu kuwa huenda utamaduni au ustadi huo wa belly dancing unakufa polepole Misri.

Pengine ni kwa kutambua hilo ndio waandalizi wa vipindi wakaona bora walete shindano la ngoma hiyo kwenye televisheni ya kitaifa kuhifadhi na kuipa umaarufu kama kitu cha asili ya Misri.

Lakini bila shaka hilo haliswihi machoni pa bodi ya kidini nchini humo na wametoa amri kipindi hicho kiondolewe mara moja .

Bodi hiyo Dar al-Ifta imesema kuonyesha watu wakinengua viono kwenye televisheni kutazorotesha maadili ya jamii na kutapelekea mwenye itikadi kali kupata visababu vya kuipaka matope Misri ili kutia doa imani ya kiislamu ya taifa hilo.

Kutokana na kauli hiyo sasa kipindi kilichoikuwa kipeperushwe hewani juzi usiku kimeahirishwa.

Ni makala moja tu ya kipindi hiyo ndiyo iliyooneshwa - Mojawapo wa waliokuwa majaji wa kupendekeza washindi kwenye kipindi hicho ni mchezaji maarufu wa densi hiyo aitwae Dina na wengi wa washindani katika mchuano huo wa belly dancing wala si raia wa Misri .
  Via: BBC

No comments:

Post a Comment