Wanafunzi na walimu wa Shule ya sekondari Simba wa Yuda wakiwa shuleni jana jioni-Picha na Damian Kageba Lupimo
Mazishi ya mwanafunzi
aliyefahamika kwa jina la Yunis Festo aliyekuwa anasoma kidato cha nne
katika shule ya sekondari Simba wa Yuda iliyoko katika kijiji cha Bulima
wilaya ya Busega yanatarajia kufanyika kesho huko Kwimba mkoani Mwanza .
Mwili wa marehemu umesafirishwa jana jioni kutoka shuleni
Yunis
Festo aliyezaliwa tarehe 26.02.1996 amefariki dunia jana saa 11
alfajiri zikiwa zimesalia saa chache tu kuanza kufanyika kwa mtihani
wa kidato cha Nne kote nchini ulioanza jana Jumatatu.
Malunde1
blog imeambiwa kuwa mwanafunzi huyo amefariki dunia jana baada ya
kukimbizwa katika kituo cha afya Bulima na wanafunzi wenzake aliokuwa
nao bwenini alipozidiwa majira ya saa 9 usiku wa kuamkia jana.
Habari zinasema kuwa mwanafunzi huyo alikuwa anaumwa kichwa na kwamba alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa Sickle Cell.
Malunde1 blog inawapa pole ndugu,jamaa na marafiki waliofikwa na msiba huo.
Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu Yunis Festo.Amina
|
No comments:
Post a Comment