Tuesday, August 12, 2014

UGONJWA WA EBOLA WAUWA PADRI MUHISPANIA

Kasisi mmoja Muhispania aliyeambukizwa virusi vya Ebola, akiwa anafanya kazi Magharibi mwa Afrika , amefariki kutokana na homa hiyo hospitalini mjini Madrid.

Zaidi ya watu 1,000 wamefariki kutokana na homa hiyo nchini Liberia, Guinea, Sierra Leone na Nigeria tangu kulipuka kwa homa hiyo mwezi Februari.

Miguel Pajares, mwenye umri wa miaka 75, alirejeshwa nchini Uhispania kutoka Liberia wiki jana na mtawa mmoja ambaye naye aliponea kuambukizwa homa hiyo.

No comments:

Post a Comment